Friday, December 12, 2014

UJIO MPYA

Wapenzi wangu wa MiGO Fam blog napenda kuwaomba radhi kwanza kwa kutokua hewani kwa kitambo kirefu. Sina sababu ya msingi hasa iliyonifanya niwe kimya kiasi hicho so nina kila sababu ya kuwaraka radhi.

NISAMEHENI JAMANI.

Ila napenda kuwaahidi ya kwanba kuanzia sasa na kuendelea niyaenselea kuwapa burudani kama kawaida yangu. Cha msingi tuombeane uzima tu.

Asanteni

Thursday, December 15, 2011

KUKATIKA KWA MPINI SIO ........ (WEMA)

Yeah wadau wa MigoFam leo nimeamua kumtupa kwenu binti wa Mzee Abraham Sepetu (Wema) kwakua ni msichana ambaye amefanikiwa kuwa gumzo sana midomoni mwa watu kutokana na kuandikwa sana katika vyombo vya Habari hususan Magazeti. Simleti kwenu kwa maana nataka nami niwe miongoni mwa waandishi wake (Wema). La hasha. Bali nataka kumpa pole na kumtakia mambo kadhaa ambayo pengine yatamweka ama kumrudisha katika heshima ambayo mimi naamini kuwa anayo ila watu walijaribu kuiteketeza tu kwa hira zao binafsi.

Wema Abraham Sepetu


1) WEWE NI MZURI - Nataka dada yangu ufahamu kuwa wewe ni mzuri na pengine zaidi ya hao wenzio ingawa sisemi kuwa wao ni wabaya.

2) UNA VIPAJI - Hili halipingiki kwani kila mtu anafahamu fika kuwa sababu ya wewe kuwa ulipo ni kutokana na vipaji ambavyo Mungu amekutunuku achilia mbali mambo yale ya mavazi hiki cha Uigizaji kinakuweka juu zaidi.

2) UNAPENDWA SANA - Kutokana na sababu nilizozitaja hapo juu watu wengi sana wanakupenda.

3) UNACHUKIWA SANA - Kutokana na sababu hizo tatu za hapo juu watu wengi pia wanakuchukia.

WEMA.
Ukiyagundua haya na kuyafanyia kazi utakuwa katika wakati mzuri sana na hakuna kitakachokusumbua katika maisha yako kwa maana safari yako ya kimaisha bado ni ndefu mno na ni ngumu mno.

Naomba nikukumbushe kitu kimoja: Miaka kadhaa iliyopita kulikuwa na skendo moja babkubwa lililomkumbaga aliyekua (Sina hakika kama bado yupo katika tasnia) muigizaji maarufu (Christina aka Sinta) na mwanamuziki maarufu ambaye naye kwa wakati huo alikua juu sana (Sir Juma Nature). Nisingependa kuingia ndani hasa kutokana na kisa cha hawa watu ila nataka nawe uchukulie mfano wao kwa maana Sinta ni kama wewe na Nature ni kama Diamond katika mkasa huu. Hii ni kama REMIX.

 Wema na Diamond wakati wa mapenzi yao
 Aliyekua muigizaji wa Kaole - Sinta


Kibla Sir Juma Nature


Najua ya kuwa ulimpenda sana Bw. Mdogo sana Diamond lakini haupaswi kulia ovyo na kujidhalilisha mbele za watu eti ndo utamfanya akuonee huruma, si kweli bali badala yake atazidi kukuona kuwa unampenda sana na kukufanya atakavyo. Amini nakwambia anaweza kukurudia na kukutema tena. Unachotakiwa ni kukaa na kuiga mfano wa dada Sinta wa kuanza maisha mapya na sio kukurupuka na kuanza mahusiano mapya na mtu yeyote eti sababu ni maarufu au ana fedha. Dada amini ya kuwa Mpenzi wako wa kweli na wa kudumu na hata wa kumpatia watoto, yupo ni kiasi cha kusubiri tu.

MAOMBI YANGU KWAKO
Sikuombea eti iwe ndio jamaa awe amekumwaga kiukweli kweli. La hasha. Ila kama itakuwa hivyo basi kama nilivyotangulia kusema, wako yupo anakusubiri ngoja ajitokeze naamini utafurahi mwenyewe. Wema wewe ni MZURI SANA.


Rahim R. Migomba

Tuesday, November 1, 2011

AMANA HAKUNA AMANI

Ama kwa hakika nina kila sababu ya kusema haya kuhusiana na Hospitali yetu ya Wilaya Ilala, Hospitali yenye majengo mazuri ambayo pia iliwahi kutembelewa na Mheshimiwa Mkubwa Ulimwenguni Bwana Bushi (Hospitali ya AMANA).

Sehemu ya mbele ya Hospitali ya AMANA

Kwa Mtazamo wa haraka unaweza sema kuwa kutokana na uzuri wa majengo yake basi kila namna ya ugonjwa ama mgonjwa utapona/atapona (kama kupona kwa mtu ni majengo) lakini hali halisi ya watenda kazi (Madaktari) si Shwari.

Kwanini nasema si shwari?

Najua kuwa pengine mara nyingi haya hutokea lakini naomba nielezee haya niliyoyaona mimi katika siku hizi za karibuni.

Mke wangu ni mjamzito, ni ujauzito wake wa kwanza hivyo humsumbua kila mara. Siku ya J2 kuamkia J3 hali yake ilikuwa mbaya sana kutokana na kuwa alikuwa na maralia hivyo alikuwa anamaumivu makali sana sehemu za kiuno na tumboni pia. pia alikua anatokwa na damu mara kwa mara kama mtu aliye kwenye Hedhi. Tukaenda Hospitali iliyokuwa karibu na mahali tunapoishi (ukonga Madafu) ambako kutokana na hali ya kiuchumi tulishindwa na kushauriwa na mmoja wa madaktari wa pale twende Amana kwa kuwa ni Hospitali ya Serikali tutapata huduma nzuri na kwa gharama tutakayoiweza.

Tumefika Amana mapema tukakuta wakifanya usafi, tukangoja mpaka Daktari akaja tukawa ni wa kwanza kuhudumiwa kwenye majira ya saa 12 hivi. Ile tunaingia kwa Daktari tu na kumweleza tatizo lililotuleta kabla hatujajieleza vyema akatupa jibu lililotushtua. Kiurahisi tu anatwambia eti Mtoto wetu amekufa na tukitaka tumpe shilingi elfu Arobaini na Tano (45,000/=) ili akamsafishe mama yake (Mke wangu) ili kuzuia asipatwe na Kansa ya kizazi. Inauma sana kwa kweli.

Kwakua niliogopa ile hali ya kuambiwa mke wangu anaweza kupatwa na Kansa nikajikuta nikiomba aheri ya pesa hiyo naye bila kuchelewa alikubaliana nami na kuchukua hela niliyokuwa nimebaki nayo ambayo ni Shs. 21,000/=. na kuniahidi kuwa anawacheki wagonjwa wawili tu kisha anakuja kutushughulikia, hivyo tutoke nje mara moja.

Kweli baada ya dakika kadhaa akaja na kutuingiza katika chumba kingine na kumuamuru mke wangu alale ili amfanyie huo usafishaji wake kitu ambacho mke wangu alikipinga vikali kitu kilichosababisha ugomvi mkali kati ya Daktari na mke wangu na mimi nisijue cha kufanya.

maamuzi ya mwisho tuliyofikia ni Daktari kuturudishia pesa yetu na kuamua kwenda kufanya Ultra Sound ili kuhakikisha kama ni kweli yule kiumbe alishakufa au la.

Nikamwomba huyo daktari aniandikie niende kwenye Ultra Sound nasi tukaenda.

Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania J.K. akimpa mawili matatu aliyekuwa Rais wa Marekani ndugu G. W. Bushi katika hospitali ya Amana. Linaloonekana kwa mbali ni jengo litumikalo kwa X-Ray, Vipimo vya Moyo na Ultra-sound.

Hali tuliyoikuta huko kwa kweli ilitutia hofu kabisa. Ingawa tulikuwa ni watu wa mwanzoni kufika hapo lakini baada ya dakika chache baadae waliongezeka watu na kufikia zaidi ya hamsini na hakuna hata mmoja aliyefanikiwa kuingia kwa daktari katika wakati muafaka. Cha kusikitisha zaidi ni kwamba hao hao madaktari walikuwa wanawaingiza watu wengine (wenye pesa nyingi) kwa mlango wa panya na kuwaacha wale waliopo kwenye foleni kwa sababu ya vijisenti vyao walivyovitoa (5,500/=).

Wagonjwa baada ya kuona imefika majira ya saa nane mchana na hakuna aitwaye wakaanza kuishiwa na imani na kuamua kupiga kelele ndipo askari walipokuja na kuuliza madaktari kulikoni na kuweka sawa mambo na kuondoka zao wakiamini kuwa pako sawa. Alitoka Daktari mmoja na kuwakemea wagonjwa eti kwa nini wameamua kupiga kelele mpaka askari wamekuja, alidai kuwa lengo la Wagonjwa hao lilikuwa ni kumfukuzisha kazi na kuwaahidi kuwaripua katika vipimo yaani atahakikisha ndani ya nusu saa atakuwa ameshawamaliza wagonjwa wote ambao idadi yao ilishafikia zaidi ya hamsini.

Ni kweli kama alivyowahaidi aliwapitisha wagonjwa hao kwenye Ultra Sound kama chupa za soda kwenye mashine za ujazo na kuhakikisha wameisha ndani ya muda mfupi.

Ndani: Alichokuwa anafanya ndani kwa mujibu wa mke wangu ni kumfokea mgonjwa kwa kumuamrisha alale na kuanza kumpaka mafuta tumboni na kisha kupitisha mashine ya Ultra Sound kama pasi ipitishwavyo kwenye nguo isipokuwa hakurudia kama ambavyo tunafanya kwenye nguo ili kuhakikisha inanyooka. Inasikitisha sana. Alichukua karatasi ya vipimo na kuweka majibu yake ambayo tuliporudi kwa daktari (yule aliyeikosa hela yetu baada ya sisi kukataa kumsafisha mke wangu) majibu yake yalikuwa ni kama ni kulipiza kisasi na si kuhudumia mgonjwa wa kawaida tena. Alisema eti tunamsumbua bure wakati huko tumboni hakuna cha mimba wala nini kuna uvimbe tu. Inauma sana kwa kweli.

Tuliondoka tukiwa na imani kuwa MIMBA kwa uwezo wa Mwenyezi Mungu bado ipo na mtoto atazaliwa bila wasiwasi wowote na wao kwa kuwa hawana utu mioyoni mwao Mungu atawaadhibu kwa hilo. Na kwa hakika imani na hospitali hiyo imenitoka kabisa.

Naomba nieleweke vyema, sina maana ya kwamba Hospitali ni mbaya La hasha bali hawa madaktari wanaichafua Hospitali yetu kwa tabia zao binafsi za kupenda pesa kuliko utu. Wanaona ni rahisi sana kwao kutoa viumbe vya Mwenyezi Mungu visivyo na Hatia kwa maslahi yao binafsi bila kujali ni muda wa miaka mingapi watu hupoteza katika harakati za kutafuta watoto. Mungu Hapendi.

AMANA JAMANI, HAKUNA AMANI




Sunday, December 26, 2010

ILIKUA NI BOXING DAY

Ni ngumu kwangu kusahau siku ambayo mdogo wangu huyu alipozaliwa kwani ninakumbuka vitu vikuu VITATU,

Kwanza: Ilikua ni siku ya pili baada ya X-Mass yaani siku ya BOXING.

Pili: Ilikua ni siku ambayo mmoja wa shangazi zangu ambaye kwa sasa ni marehemu (Mungu amlaze mahala pema peponi, Amin) alipokua anaolewa.

Tatu: Ni siku ambayo mimi na baba tulikua bize Town tukitafuta aina gani ya TV inatufaa, ikumbukwe suala la TV lilikua ni adimu sana TANZANIA. Tulifanikiwa kurudi na TV ya Black n White iliyokua na jumba lenye rangi nyekundu.

HAPPY BIRTHDAY BROO
MUNGU akupe maisha marefu na yenye baraka tele. AMIN.

Monday, December 13, 2010

NJEMBA YABAMBWA IKICHEZA VIDUKU KWENYE DALADALA

Jamani jamani jamani! hivi hii hali itaisha lini? Hivi ni nani wa kulaumiwa katika hili?

Kituo cha daladala Ubungo.

Hapa ni sehemu ambayo daladala nyingi ziendazo sehemu mbalimbali za nje na ndani ya jiji la Dar es Salaam zinapoanzia safari yake. Watu huchukua usafiri wa kuelekea waendako toka hapa na hakuna kati yao atakayejua nini kitatokea ndani ya usafiri  (Daladala) aliouchukua. Jamani ndani ya Daladala kuna mengi mno, kati ya hayo yapo mazuri kwa maana watu tofauti hupata nafasi ya kujadili na mada tofauti zihusuzo jamii na mbalimbali yanayowazunguka. HILI ni moja kati ya mambo mazuri.

Daladala aina ya DCM ikitokea Mbagara kuelekea Kivukoni.

Jambo baya huwa ni pale ambapo mmoja kati ya abiria waliopanda ndani ya daladala hilo anapoamua kuonesha kipaji chake cha kucheza na mifuko ya abiria wengine kana kwamba ana ruhusa ya kufanya hivyo. Usipokua makini utajikuta hata ile nauli uliyotegemea kulipia usafiri huo imechukuliwa na Abiria huyu asiye na wema hata theluthi (KIBAKA).

Abiria wakiwa wamejaa kwenye DCM huku wengine wakiwa wamesimama katika style wanayoiita 'KUPIGA RANGI' 

Kutokana na utofauti wa binadamu katika kukidhi haja zao, kila mmoja na njia tofauti na mwingine katika hili. Kuna watu ambao hupanda madaladala si kwa nia ya kuwahi kazini au kuiba kitu cha mtu mwingine La, Hasha! Wao hupanda Daladala na hasa zilizojaa tu ili waweze kujipa burudani ya KIMWILI. Watu hawa ni maarufu sana kwa jina la 'DUNGADUNGA'

Leo nimepata MOOD ya kuyaandika haya ili kuwatahadharisha watu hasa akina dada juu ya hawa watu. Haya yametokea leo wakti nikitokea nyumbani kwangu kuelekea kazini. Kuna njemba moja almanusura aambulie Kichapo kwa sababu ya kucheza KIDUKU nyumba ya mgongo wa dada fulani aliyekuwemo kwenye daladala tuliyoipanda. Jamaa huyo mtanashati ambaye kwa sura ni mzuri na angeweza kumnasa msichana yeyote ambaye angemtaka ameshindwa kufanya hivyo badala yake ameamua kuwa anamalizia shida zake kwenye madaladala yaliyojaa.

Kisa kilikua kama ifuatavyo: Jamaa amepanda kwenye gari kwa kuikimbilia kwa sababu tayari ilikuwa imeshajaa na abiriria wengi walikua wamesimama. Kwa mwendo wa kutoka Banana hadi maeneo ya TAZARA jamaa alionekana akicheza viduku taratibu kwa kumfuata dada wa watu kila hatua aliyosogea. Kumbe kitendo kile kilishuhudiwa vyema na Kondakta wa daladala hiyo ambaye aliamua kunyamaza kimya, (SIKUJUA aliogopa nini). Mbali na kondakta kuna jamaa mwingine ambaye pia alipata bahati ya kuliona hilo lakini alishindwa kuvimilia na kujikuta akimhoji jamaa kwa ukali kuwa alikuwa anataka nini kwa dada huyo (MDUNGWAJI). Jamaa kwa kujiuma uma alijibu kitu ambacho hakikueleweka kitu ambacho kiliamsha hisia za watu karibu wote kwenye daladala hiyo pamoja yule dada (MDUNGWAJI) mwenyewe ambaye kwa mara ya kwanza alisikika akisema, "mi nimemuona muda mrefu akinifuata fuata huku nyuma ila sikujua alikua anafuata nini", alisema dada huyo huku akiendele kuwa baada ya ahapo alisikia kama aliyeloana sehemu zake za MCHINA. Maneno ya dada huyu yaliamsha hisia za Abiria wengine ambao wengine walimuomba kondakta amlete Jamaa huyo (MDUNGAJI) huku nyuma (tulipokuwa tumekaa sisi) ili naye ADUNGWE.

Kwa bahati nzuri kabla ya maamuzi hayo kufikia muafaka jamaa alishuka maeneo ya MTAVA na kupanda daladala jingine ambayo hatukujua kama aliendelea na VIDUKU ama alikoma.

JAMANI mbona mademu wako wengi VIDUKU kwenye daladala vya nini?

Friday, November 5, 2010

Najaribu kuvuta picha ya miaka kadhaa tulipokuwa tukitoza ushuru kule shule ya Msingi Uhuru Mchanganyiko, sikutegemea kama kuna siku tungekuwa separate way lakini poa tu ndo maisha yanavyotaka. Nakumic sana best yangu Law.
Sharobalo LAW MBETENI katika poz.

 Unanikumbusha kwa Mzee KIJINO







Friday, October 15, 2010

MUNGU AMLAZE MAHALA PEMA MAMA YANGU. AMEN

Ukweli ni kwamba tulimpenda sana, lakini Muumba alimpenda zaidi na mapenzi yake ni lazima yatimie. Ni miezi miwili sasa tangu amefariki lakini machungu tuliyonayo kwa kuondoka kwake ni makubwa kama vile ametutoka jana. MUNGU amlaze mahala pema peponi mama yangu mpendwa. AMEN.
MAREHEMU MAMA YANGU (BI. HABIBA CHUGULO) WAKATI WA UHAI WAKE